Beki wa Chelsea afungiwa

Chama cha soka England FA leo kimetangaza maamuzi mazito kwa beki wa kimataifa wa Hispania anayeichezea Chelsea ya England Marcos  Alonso baada ya kukutwa na hatia ya kosa la kumchezea faulo ya makusudi mchezaji wa Southampton Shane Long.

FA jana wametangaza kuamua kumfungia mechi tatu Marcos Alonso baada ya kumkuta na hatia na kugundua kuwa Marcos alifanya kwa makusudi kumkanyaga Shane Long na kukusudia kumuumiza, kabla ya adhabu hiyo kutolewa Marcos alipewa muda hadi jana Jumatano ya  April 18 saa 20:00 ajitetee kwa nini asiadhibiwe.

Beki wa Chelsea Marcos Alonso aliingia matatizoni Jumamosi ya April 14 2018 katika mchezo kati ya Chelsea dhidi ya Southamton uliyomalizika kwa Chelsea kupata ushindi wa magoli 3-2, baada ya kumchezea faulo  Shane Long.

Leave a comment